AFCON 2015:MALAWI NA RWANDA ZA FUZU HATUA ZA MAKUNDI KWA PENATI.

Malawi wamefuzu hatua makundi ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika,AFCON 2015 nchini Morocco baada ya kifunga benin kwa mikwaju 4-3 ya penalti 



Mechi hiliyo pita mjini cotonou ,malawi walifungwa goli 1-0  na leo wakiwa nyumbani wamepata ushindi wa aina hiyo hivyo sheria ya mikwaju ya penalti kuamua kupata mshindi.

Bao pekee la malawi lilifungwa na John banda katika dakika ya 43 

Malawi ambao wako nafasi ya 16 katika nchi za Afrika kwenye viwango vya Fifa walitawala mchezo kwa mda mrefu.

wakati huo nao rwanda wamefuzu hatua ya makundi kwa mkwaju ya penalti baada ya kufuta kipigo cha mabao 2-0 walichopta ugenini zidi ya Congo -Brazzavile 

mabao mawili ya Rwanda yalipatikana kunako kipindi cha pili kupitia kwa ndahinduka michael katika dakika ya 55na meddy kagere katika dakika ya 60 na kuipa ushindi nchi hiyo.

Rwanda walishinda penalti 4-3 na patrick Sibomana alifunga penalti ya ushindi na sasa wanaungana na mabingwa watetezi Nigeria ,Afrika kusini ,na Sudan katika kundi A.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment