GARI LA RAIS LILILOIBWA KENYA LAPATIKANA UGANDA



gari
Jumatano ya wiki iliyopita ndio liliibwa hili gari aina ya BMW lisilopenya risasi ambalo huwa linakuwepo kwenye msafara wa Rais Kenyatta, na taarifa ya Ikulu ilisema liliibwa wakati dereva wake ambae ni askari alikua akielekea kwenye makazi ya Polisi Nairobi, njiani akasimamishwa na watu waliokuwa na AK 47 wakamtupa mtaroni baada ya kumvua nguo na kukimbia nalo.


Taarifa mpya ambayo inaripotiwa na Julius Kepkoich toka Kenya inasema gari hili limepatikana kwenye mji wa Tororo Uganda na tayari limepelekwa Kampala baada ya msako uliofanywa na Polisi na kumkamata mshukiwa mmoja hotelini mjini Bungoma.


Kikosi cha Polisi wa Flying squard kikishirikiana na Interpol walivuka boda na kuingia mji wa Tororo Uganda walikohisi kwamba ndiko kulikopelekwa gari hilo.


Polisi wanamshikilia Nelson Topicho aliyekamatwa Bungoma na anatarajiwa kurejeshwa Nairobi ili kuhojiwa zaidi ambapo kikosi kingine cha Nakuru Kenya kinamshikilia Agrey Odhiambo anaetuhumiwa kukarabati gari lililoibwa na kumiliki bunduki huku Nairobi wakitarajiwa kumuhoji upya dereva wa Ikulu David Muchui.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment