Kikao cha Nato: Urusi yashutumiwa.


Katibu Mkuu wa NATO Anders Fogh Rasmussen
Viongozi wa nchi za Magharibi wameishutumu Urusi kwa "ushawishi" wake katika mgogoro wa Ukraine, mwanzoni mwa mkutano wa viongozi wa Nato huko Wales, Uingereza.
Nato na Uingereza zimeonya kuwa shinikizo juu ya Urusi litaongezeka iwapo haitabadili msimamo wake kuhusu eneo la mashariki mwa Ukraine.
Rais wa Ukraine atawapa taarifa viongozi wa Marekani na Ulaya kuhusu mazungumzo ya awali kati yake na Rais Vladmiri Putin wa Urusi juu ya mpango wa kusitisha mapigano nchini Ukraine.
Kikao cha viongozi wa Nato, Wales, Uingereza
Watu wapatao 2,600 wamekufa katika vita kati ya majeshi ya Ukraine na waasi.
Nchi za magharibi zinasema zina ushahidi kwamba Bwana Putin anawaunga mkono wapianzani wanaotaka kujitenga kutoka Ukraine kwa kuwapa mafunzo ya kijeshi na silaha, lakini Urusi inakana tuhuma hizo.
Kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa zaidi ya watu milioni moja wamelazimika kuyakimbia makaazi yao mashariki mwa Ukraine.
Mkuatano huo wa siku mbili mjini Newport utatawaliwa na mjadala kuhusu mgogoro wa Ukraine.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment