Wazazi wa Sotloff watoa kauli yao


Steven Sotlof
Familia ya mwandishi wa habari Steven Sotloff hatimaye imezungumza kwa mara ya kwanza tangu mtoto wao auawe na wapiganaji wa dola ya Kiislam IS na picha za mauaji hayo kuonyeshwa.
Akizungumza kwa niaba ya familia hiyo, Barak Barfi kutoka taasisi ya America Foundation think tank akiwa nyumbani kwao Pinecrest, Florida amemuelezea Sotloff kuwa ni mtu aliyefanya kazi yake kwa niaba ya wanyonge wa Mashariki ya kati.
Wanafamilia hao wamesema mtoto wao hakuwa tu shujaa bali ni wa namna yake ambaye daima alikuwa akitafuta kurejesha nuru palipo na giza.
Hata hivyo wazazi hao wa Steven walitoa heshima zao pia kwa kifo cha James Foley aliyechinjwa pia na wapiganaji hao wa dola ya Kiislam ya IS.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment