Juhudi za Marekani kukusanya uungwaji mkono wa kimataifa kwa kampeni yake ya kijeshi dhidi ya kundi linalojiita "Dola la Kiislamu" zinaonekana kuendelea kuzaa matunda kwa washirika kadhaa kujiunga nazo.
Ndege ya Rais Francois Hollande wa Ufaransa ikiwa na shehena ya tani 15 za msaada wa kibinaadamu utakaopelekwa mji mkuu wa Kurdistan baadaye leo, imewasili Baghdad, ikiwa ni ziara ya kwanza ya mkuu wa nchi tangu kutangazwa kwa serikali mpya nchini Iraq. Hollande anaambatana na waziri wake wa ulinzi, Jean-Yves Le Drian, na wa mambo ya nje, Laurent Fabius.
Juzi Jumatano, Fabius alitangaza nchi yake iko tayari kushiriki kwenye operesheni ya kijeshi ya Marekani dhidi ya kundi la Dola la Kiislamu, siku moja kabla hata Rais Obama hajatoa hotuba yake iliyofungua njia kwa mashambulizi hayo.
0 maoni:
Post a Comment