Mashambulizi dhidi ya 'Dola la Kiislamu' yaiva


Juhudi za Marekani kukusanya uungwaji mkono wa kimataifa kwa kampeni yake ya kijeshi dhidi ya kundi linalojiita "Dola la Kiislamu" zinaonekana kuendelea kuzaa matunda kwa washirika kadhaa kujiunga nazo.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry (kushoto) katika mkutano na washirika wa mataifa ya Kiarabu. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry (kushoto) katika mkutano na washirika wa mataifa ya Kiarabu.
Katika kile kinachoonekana kuwa matayarisho rasmi ya kulishambulia kundi hilo ndani ya ardhi ya Syria na Iraq, kufuatia hotuba ya jana ya Rais Barack Obama hapo jana, Rais wa Ufaransa amewasili Iraq hivi leo (12 Septemba), huku Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry, akiendelea na ziara ya kusaka uungwaji mkono katika nchi za Kiarabu, nayo Australia ikitangaza hali ya tahadhari kutokana na uwezekano wa mashambulizi kutoka wanachama wa Dola la Kiislamu kwenye ardhi yake.
Ndege ya Rais Francois Hollande wa Ufaransa ikiwa na shehena ya tani 15 za msaada wa kibinaadamu utakaopelekwa mji mkuu wa Kurdistan baadaye leo, imewasili Baghdad, ikiwa ni ziara ya kwanza ya mkuu wa nchi tangu kutangazwa kwa serikali mpya nchini Iraq. Hollande anaambatana na waziri wake wa ulinzi, Jean-Yves Le Drian, na wa mambo ya nje, Laurent Fabius.
Juzi Jumatano, Fabius alitangaza nchi yake iko tayari kushiriki kwenye operesheni ya kijeshi ya Marekani dhidi ya kundi la Dola la Kiislamu, siku moja kabla hata Rais Obama hajatoa hotuba yake iliyofungua njia kwa mashambulizi hayo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment