SMZ yapinga kuwepo kwa ubaguzi katika kutowa miche ya Mikarafuu kwa Wakulima

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema haina Ubaguzi wa aina yoyote katika kugawa Miche ya Mikarafuu badala yake inaangalia namna ambavyo Mkulima katayarisha mashamba yake kwa ajili ya kupanda zao hilo.

Afisa kutoka Kitengo Dhamana cha Utoaji wa Miche ya Mikarafuu Badru Kombo Mwenvura ameyasema hayo wakati alipokuwa akijibu tuhuma zilizotolewa na Wakulima wa Karafuu katika kijiji cha Mkwajuni Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Amesema si kweli kuwa Miche hiyo hutolewa kwa misingi ya itikadi ya Vyama na kwamba Kitengo husika cha kutoa Miche ya Mikarafuu huitoa kwa Mkulima yoyote aliyekamilisha masharti.

“Kwa kweli lazima tuweke wazi kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar haijadhamiria kuwabagua wananchi wake na hasa Wakulima wa Zao la Karafuu katika kuwapatia Miche.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment