Madereva walioendesha wakiwa mtungi siku ya mwaka mpya wajikuta mbaroni


 

Madereva kibao wamekamatwa jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kuendesha magari huku wakiwa wamelewa katika sikukuu ya mwaka mpya.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema walifanya operesheni dhidi ya madereva na kuwabaini madereva hao wamekuwa wanakunywa huku wakiendesha ambapo ni kinyume na sheria.

“Sasa hivi tukimkamata dereva akiwa amelewa hatumuandikii faini ya kulipa tumeona wengi tumeona wengi wao wameona rahisi kuendelea kurudia makosa,hivyo tunawapeleka mahakamani sheria ichukue mkondo wake,” alisema Kamanda Sirro.

Aidha Kamanda Sirro alisema katika operesheni hiyo waliwakamata madereva 10 Temeke,15 Kinondoni na Ilala 4 . 

BY:EMMY MWAIPOPO
CHANZO: MWANANCHI
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment