Mauaji ya waziri wa mazingira: Watu watatu wakamatawa


mediaPolisi ikipiga doria katika moja ya mitaa ya mjini Bujumbura,
Polisi ya Burundi imesema kuwa imewakamata watu watatu ikiwa ni pamoja na mwanamke mmoja ambao inawashtumu kuhusika katika mauaji ya Waziri wa Maji na Mazingira Emmanuel Niyonkuru. 
Waziri wa Maji na Mazingira Emmanue Niyonkuru aliuawa usiku wa kuamkia Jumapili Januari 1, 2017 alipokua akiingia kwa gari nyumbani kwake katika kata ya Rohero katikati mwa mji wa Bujumbura, kwa mujibu wa polisi, huku ikiongeza kuwa aliyetekeleza mauaji hayo hajulikani aliko.
Manispa ya jiji la Bujumbura inabaini kwamba mauaji ya Waziri Emmanuel Niyonkuru yaliendeshwa saa saba usiku za Afrika ya Kati.
Inaarifiwa kuwa Waziri Niyonkuru aliuawa kwa bastola.
Msemaji wa polisi Pierre Nkurikiye ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa polisi inamshikilia mwanamke aliyekua akiambatana na Waziri Niyonkuru kwa ajili ya uchunguzi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment