Rais John Pombe Magufuli leo tarehe 1/1/ 2017 ametengua uteuzi  uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania 9TANESCO) Mhandisi Felchesmi Mramba na kumteua Dk Tito Esau Mwinuka kuwa Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO Mhandisi Felchesmi Mramba
Akiwa mkoani Kagera leo Rais Magufuli alisikika akisema kuwa haiwezekani mtu mmoja kutokana na nafasi yake afanye maamuzi ya kupandisha umeme huku akitambua kuwa kufanya hivyo ni kuwaumiza watanzania na kuahidi kuendelea kuwatumbua wafanyakazi wa Serikali ambao ni majipu. 
Kwa mwaka 2017 Mkurugenzi wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba anakuwa mfanyakazi wa kwanza kutumbuliwa na Rais John Pombe Magufuli