Ujumbe Manji aliotuma kwenda Yanga akiwa wodini

Mwenyekiti wa Kkabu ya Yanga, Yusuf Manji amemtaka nahodha wa klabu hiyo na uongozi mzima kuhakikisha kuwa wanapambana mwanzo mwisho na kuwa matatizo yake yasiwapotezee muda.
Manji alitoa maneno hayo juzi alipokuwa bado yupo Hospitali ya Taifa Muhimbili katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alipokuwa akipatiwa matibabu. Akiwa hospitalini hapo alipata ugeni wa viongozi wa Yanga walioambatana na nahodha wa klabu hiyo kwa ajili ya kumjulia hali.
Ugeni huo alikuwemo pia kiongozi na mwakilishi wa wachezaji ndani na nje ya uwanja, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na msaidizi wake Haruna Niyonzima ulifika hospitali hapo maratu baada ya kutua kutoka Comoro walikokwenda kucheza mchezo wa Klabu Bingwa Afrika na kufanikiwa kupata ushindi wa 5-1.
Manji aliwaambia kuwa matatizo yake yasiwahusu hata kidogo kwani wanachotakuwa kukifanya ni kuhakikisha wanapambana kila anayekuja mbele yao apigwe goli nyingi za kutosha. Aidha, Manji aliwapongeza kwa ushindi walioupata Comoro na kutakiwa kushikilia hapo hapo bila kuyumbishwa na chochote.
Manji alitoka jana hospitalini hapo alipokuwa wamelazwa baada ya kupata matatizo ghafla akiwa Kituo cha Polisi cha Kati, Dar es Salaam anaposhikiliwa kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.
Chanzo: Mwanaspoti

from Blogger http://ift.tt/2lUAWKc
via IFTTT


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment