Wafanyakazi 25 wa Quality Group kujieleza leo katika ofisi za uhamiaji

Hivi karibuni mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuf Manji, alituhumiwa na ofisi ya uhamiaji kuajiri wafanyakazi 25 wa kampuni yake ya Quality Group wanaowafanya kazi bila vibali. Leo wafanyakazi hao wataanza kujieleza kwa maandishi katika ofisi za uhamiaji.
Ofisa uhamiaji Mkoa, John Msumule amesema uhamiaji haijawakamata wafanyakazi hao, isipokuwa inashikilia hati zao za kusafiria.
Alisema “Kesho yaani (leo) tunatarajia kuanza kuwahoji ili watoe maelezo yao, ikiwa ni hatua ya maandalizi ya kuwapeleka mahakamani Jumatatu ili kuwezesha hatua nyingine za kisheria kuchukua nafasi yake.”
Sambamba na kuhojiwa kwa wafanyakazi hao, Manji anasubiriwa na kushtakiwa kwa madai ya kuajiri wageni wasiokuwa na vibali vya kufanya kazi nchini.

from Blogger http://ift.tt/2lO8UUC
via IFTTT


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment