SIASA ISIWE CHANZO CHA KUARIBU MAENDELEO JIJINI MBEYA.




Meya wa jiji la Mbeya David Mwashilindi amewataka Viongozi pamoja na wananchi kutoharibu maendeleo kwa itikadi za kisiasa.



Hayo ameyasema wakati akiweka jiwe la msingi la zahanati katika kata ya Tembela na Mwasanga ambapo amesema kuwa wakati huu sio wa siasa bali ni wakati wa kufanya maendeleo.

Awali akisoma risala kwa mgeni rasmi afisa mtendaji wa kata ya Tembela Obel Yesaya amesema kuwa ujenzi wa zahanati hiyo ni kwa ushirikiano wa kata mbili ambao ulianza  February mwaka 2016 na ujenzi huo ni kwa nguvu ya wananchi ambao wamechangia jumla ya shilingi million 9.

Akijibu  risala hiyo  Mwashilindi amewataka viongozi kujikita katika maendeleo ya ujenzi wa zahanatu pasipo kuangalia itikadi zao za vyama na amechangia tani moja ya simenti ili kukamilisha ujenzi.

Naye mwenyekiti wa wilaya Chadema Obadia Mwaipalu amesema kuwa ili ujenzi wa zahanati uweze kukamilika unahitaji umoja na mshikamano.

Kwa upande wao madiwani wa kata hizo mbili Diwani Joel Okoka (CCM) na Andason Ngao (CHADEMA) wamesema kuwa  wao ni vyama tofauti lakini wamesema utofauti wa vyama hawawezi kuuingiza katika suala la maendeleo.

Nao wananchi wa maeneo hayo wameshukuru kwa kuweza kuanza ujenzi wa zahanati hiyo kutokana na huduma hiyo kuwa mbali na wanawake wamekuwa wakipata shida wakati wa kujifungua na wakati mwingine kujifungulia njiani.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment