Beki wa Simba Abdi Banda hivi
sasa yupo huru kuitumikia klabu yake ya Simba baada ya leo adhabu yake
kutangazwa kumaliza kutumikia adhabu yake . Mchezaji huyo alifungiwa na
Bodi ya Ligi baada ya kumpiga ngumi mchezaji wa Kagera Sugar, George
Kavila
Abdi Banda
Kamati ya nidhamu ilikaa siku ya jana na
wakati inakaa tayari mchezaji huyo alikuwa amekosa mechi mbili hivyo
kamati ilipitia na kusikiliza pande zote mbili na kufanya maamuzi kuwa
zile mechi mbili ambazo mchezaji huyo alizikosa ndiyo adhabu yake tosha
kwa kosa alilofanya.
Awali mchezaji huyo baada ya kufanya
tukio hilo ambalo mwamuzi hakuliona, alisimamishwa kucheza ligi kuu
kusubiri maamuzi, na akakosa michezo dhidi ya Mbao FC na Toto Africans.
Mchezaji huyo wa Simba ataungana na
wachezaji wengine wa klabu hiyo ambao wataingia kambini siku ya Jumapili
kujiweka sawa dhidi ya mechi zilizobaki kwenye Ligi Kuu Bara ambazo
zinaendelea nchini.
0 maoni:
Post a Comment