Marekani iko tayari kufanya mazungumzo na Korea Kaskazini lakini…






Marekani iko tayari kwa mazungumzo na Korea Kaskazini yenye lengo la kuondoa zana za nuklia kutoka eneo hilo, kwa mujibu wa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani, Rex Tillerson.

Aidha alisema kuwa, Marekani itatumia nguvu za kijeshi ikiwa itahitajika.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa China, mshirika mkubwa wa Korea Kaskazini, anasema makubaliano ya amani ndio njia pekee.
Bwana Tillerson aliliambia baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa kuwa, tishio la Korea Kaskazini ni kushambulia majirani zake kwa zana za nuklia.
Maelfu ya wanajeshi wa Marekani wako nchi majirani wa Korea Kaskazini ikiwemo Korea Kusini na Japan.
Tillerson amezitaka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, kuiwekea Korea Kaskazini vikwazo na kupunguza uhusiano wao wa kidiplomasia na nchi hiyo.
“Kwa miaka kadha Korea Kaskazini imekuwa ikiendesha kwa nguvu ya mabavu, na huu ni mpango hatari.”
“Ni wakati wetu kuchukua hatua na kudhibiti hali,” Tisho la Korea Kaskazini la kufanya shambulizi la nuklia dhidi ya Korea Kusini au Japan ni la kuwezekana, na ni muda tu kabla ya Korea Kaskazini kufanikiwa kupata uwezo wa kushambulia Marekani.” alisema Tillerson.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment