Mpira wa wavu katika kituo cha nuklia Korea Kaskazini?

Wataalam wa Marekani wanaochanganua picha za setlaiti kutoka Korea Kaskazini wanasema kuwa wameona kitu kisichokuwa cha kawaida katika kituo cha nuklia cha taifa hilo: Uwanja wa mpira wa wavu.
Haki miliki ya picha Digitalglobe/Getty Images
Image caption Picha za setlaiti zinaonyesha kwamba mchezo wa mpira wa wavu unaendelea
Picha hizo zilichukuliwa siku ya Jumapili na setlaiti moja ya kibiashara huku kukiwa na uvumi kwamba Pyongyang ilikuwa inajiandaa kufanya jaribio la sita la kombora la kinyuklia wakati ambapo kuna wasiwasi kati yake na Marekani.
Picha hizo zilitolewa na 38 North, mradi wa kuchunguza wa Korea kaskazini katika chuo kikuu cha Johns Hopkins huko Maryland.
Wachanganuzi hao walitoa sababu mbili kwa yaliokuwa yakitendeka katika kituo hicho cha Punggye-ri: Huenda maandalizi yalikuwa yamesitishwa ama ni mpango wa udanganyifu unaofanywa na serikali.
Hatahivyo walisema katika ripoti yao, kwamba kituo hicho cha Punngye kiko tayari kuandaa jaribio la sita la nyuklia wakati wowote ule wakati agizo litakapotolewa kutoka Pyongyang.
Hadhi ama uwezo wa kituo hicho haijulikani ,mtaalam Joseph S Bermudez Jr, Jack Liu na Frank Pabian walisema.
Maelezo ya vitendo vya hivi karibuni yanasema kuwa kituo hicho na maandalizi yake ya kufanyia majaribio kombora la sita la nuklia yamesitishwa kwa muda huku wafanyikazi wakiruhusiwa kwenda mapumziko.
Pyongyang imesitisha vitendo vyake katika kituo hicho kama mpango wake wa kimkakati na kuchelewesha jaribio hilo la kombora la sita la kinyuklia hadi wakati ambapo utibuzi wake utalipatia fursa ya kisiasa.
Haki miliki ya picha Digitalglobe/Getty Images
Image caption Picha za setlaiti zinaonyesha kwamba mchezo wa mpira wa wavu unaendelea katika kituo cha kinyuklia nchini Korea Kaskazini 
 
 
 
Picha za setlaiti zinaonyesha kwamba mchezo wa mpira wa wavu unaendelea katika kituo cha kinyuklia nchini Korea Kaskazini
 
Picha hizo zinaonyesha uchimbaji uliokua ukiendelea ambao huenda ukaonyesha kwamba kulikuwa na uchimbaji wa mahandaki lakini hakujakuwa na utoaji wa maji katika mahandaki hayo yanayotumika kufanyia jaribio kombora la kinyuklia.
Kumekuwa na uvumi kwamba kiongozi wa taifa hilo Kim Jong un huenda akatoa agizo la kombora hilo la kinyuklia ili kwenda sambamba na maadhimisho ya 105 ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa taifa hilo Kim 11-sung Jumamosi iliopita.
  • Je ulimwengu utafanyaje?
Kumekuwa na wasiwasi hivi karibuni huku Pyongyang ikionya Washington kutofanya uchokozi katika jimbo hilo, ikisema iko tayari kulipiza kwa shambulio la kinyuklia.
Marekani, kwa upande wake inasema kwamba wakati wa subira ya kimkakati dhidi ya Korea Kaskazini umekwisha.
Kituo hicho cha Pungye kiko katika eneo la milima kaskazini mashariki.
Korea Kaskazini inasema kuwa imefanya majaribio matano ya kinyuklia mwaka 2006, 2009, 2013 na mwezi Januari pamoja na Septemba 2016.
Lakini swali ni je taifa hilo limepiga hatua gani katika mpango wake wa kinyuklia?.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment