Man City marufuku kusajili miaka miwili



Klabu ya soka ya nchini Uingereza, Manchester City, imefungiwa kusajili na bodi ya ligi ya nchini hiyo vijana wadogo walio na umri wa chini ya miaka 18 sambamba na kutozwa faini ya Paundi 300,000 kwa kuvunja sheria ya maendeleo ya vijana.
Kufuatia uchunguzi wa Bodi ya Ligi Kuu, ushahidi umepatikana kwa City wamevunja sheria za Ligi.

Uvunjaji huo wa sheria unahusu kufanya mazungumzo na wachezaji wawili wa academy tofauti kwa ajili ya kuwasajili huku wakiwa wamesajiliwa na klabu nyingine.
Adhabu hiyo ni sawa na waliyopewa Liverpool mwezi uliopita baada ya kukutwa na hatia ya ‘kuiba’ mchezaji mwanafunzi wa shule wa Stoke City.

Kuwasiliana na mchezaji wa academy yoyote akiwa amesajiliwa na klabu yake ya wakati husika ni kosa, ambalo City wamefanya na sasa linawagharimu.
BY HAMZA FUMO
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment