Rais Trump atuma salaam za Eid al Fitr kwa waislam duniani


mediaRais wa Marekani Donald TrumpReuters/路透社
Waislam katika eneo zima la Mashariki ya Kati wanasherehekea siku ya kwanza ya Eid al-Fitr, sikukuu inayoashiria mwisho wa mwezi mtukufu wa Ramadan.
Rais wa Marekani Donald Trump ametuma salamu za Eid kwa waislam wote wanaoadhimisha sikukuu hii,akikumbusha umuhimu wa huruma na wema huku utawala wake ukivunja desturi ya kuandaa shughuli ya kutambua kumalizika kwa mwezi Mtukufu
Trump amesema kuwa pamoja na waislamu duniani kote , Marekani inakumbuka wajibu wake kuheshimu matendo ya huruma na wema
Tangu utawala wa Bill Clinton Marekani imekuwa na desturi ya kuandaa tukio kuashiria sikukuu ya Eid al Firt
Wakati huo huo Vikosi vya usalama vya ufilipino vimetangaza saa nane za kusitisha mapigano leo Jumapili, katika opelesheni yake inayoendelea dhidi ya wanamgambo wa kiislma wanaodhibiti mji wa Marawi ili kuruhusu wakaazi wa mji huo kusherehekea Eid al Fitr.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment