Hawa ndio wa kuu wa mikoa Tanzania bara kuanzia machi hii, Makonda na wengine wachache wapya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.

Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam.

 Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo;

Mh. Paul Makonda – Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.

Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga – Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu – Mkuu wa Mkoa wa Kagera.

Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga – Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga – Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Mh. Godfrey Zambi – Mkuu wa Mkoa wa Lindi.

Dkt. Steven Kebwe – Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven – Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.

Mh. Anna Malecela Kilango – Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

10.  Mhandisi Methew Mtigumwe – Mkuu wa Mkoa wa Singida.

11.  Mh. Antony Mataka – Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.

12.  Mh. Aggrey Mwanri – Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

13.  Mh. Martine Shigela – Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

14. Mh. Jordan Mungire Rugimbana – Mkuu wa Mkoa Dodoma.

15. Mh. Said Meck Sadick – Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.

16. Mh. Magesa Mulongo – Mkuu wa Mkoa Mara.

17. Mh. Amos Gabriel Makalla – Mkuu wa Mkoa Mbeya.

18. Mh. John Vianey Mongella – Mkuu wa Mkoa Mwanza.

19. Mh. Daudi Felix Ntibenda – Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

20. Mh. Amina Juma Masenza – Mkuu wa Mkoa wa Iringa.

21. Mh. Joel Nkaya Bendera – Mkuu wa Mkoa wa Manyara.

22. Mh. Halima Omary Dendegu – Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.

23. Dkt. Rehema Nchimbi – Mkuu wa Mkoa wa Njombe.

24. Mhandisi Evarist Ndikilo – Mkuu wa Mkoa wa Pwani.

25. Mh. Said Thabit Mwambungu – Mkuu wa Mkoa Ruvuma.

26. Luteni Mstaafu Chiku Galawa – Mkuu wa Mkoa wa Songwe (Mkoa mpya).

Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa, wataapishwa Jumanne tarehe 15 Machi, 2016 saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Jijini Dar es salaam.

Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU

Dar es salaam

13 Machi, 2016

from Blogger http://ift.tt/1QX27fO
via IFTTT


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment