MSANII PAM D ASTUKIA WANAUME KUMLEMAZA


 
Pam D

Binti ambaye sasa hakamatiki kwenye ulimwengu wa muziki Bongo, Pam D amefunguka kuwa, sasa hivi anasitisha kolabo na wasanii wa kiume akiwemo yule aliyemtoa, Mesen Selekta akidai kuwa amegundua wanamlemaza.
Akifungukia muziki anaofanya kwa sasa, Pam D alisema, anajua anacho kipaji na anaweza kusimama yeye kama yeye hivyo ni wakati wake sasa wa kutoa ngoma zake kali.
“Siwezi kukataa, Mesen kanipa sapoti kubwa sana mpaka kufikia hapa lakini sasa nimeona nisimame mimi kama mimi nione nitafika wapi, unajua wakati mwingine ukishirikisha sana wasanii waliokutangulia, hasa wanaume unajilemaza, kipaji chako kinashindwa kuonekana vizuri,” alisema Pam D.
Kwa sasa mwanadada huyo anaandaa ngoma yake mpya baada ya kufanya poa na traki zake zilizotangulia kama vile Popolipopo na Nimempata.

from Blogger http://ift.tt/1Z9bv5q
via IFTTT


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment