Vita Dhidi ya Madawa ya Kulevya..Wanawake Wawili Wadakwa na Kilo 114 za Bangi..!!

Wanawake wawili ni miongoni mwa watu zaidi ya 15 waliokamatwa kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya mkoani Mwanza
Watu hao wamekamatwa wakijihusisha nadawa hizo ndani ya wiki moja kuanzia Febuari 6.
Habari zinasema wanawake hao wamekamatwa wilayani Magu wakiwa na kilo 114.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema watuhumiwa 11 wamekamatwa wilayani Nyamagana na Ilemela na kilo 57 za dawa za kulevya aina ya miraa na kete mbili zinazodaiwa kuwa ni heroin.
“Mtuhumiwa mwingine ambaye ni mfanyabiashara wa vipuri vya magari, alikamatwa eneo la Butimba akiwa na kete 240 ya dawa za kulevya zinazodaiwa kuwa ni heroin na ndunga mbili,” amesema.
Msangi amesema mtuhumiwa huyo alitaka kuzitumbukiza chooni dawa hizo ili kupoteza ushahidi, lakini polisi waliwahi kukata bomba.

from Blogger http://ift.tt/2lDvhrW
via IFTTT


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment