BANDARI YA MALINDI INAKUMBWA NA TISHIO LA KUINGIZA BIDHAA HARAMU



NAIBU Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mohammed Ahmada amekiri kuwepo kwa udhaifu wa ukaguzi wa mizigo ya abiria katika bandari ya Malindi wakati wanapoingia nchini kutoka sehemu nyingine na kuwepo tishio la kuingiza bidhaa na vitu mbalimbali haramu.


Ahmada alisema hayo wakati alipozungumza na viongozi wa Shirika la Bandari na wakuu wa vyombo vya ulinzi katika ziara ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yussuf Masauni katika eneo la Bandari ya Malindi.

Alisema kuanzia sasa utafanyika ukaguzi na kuhakikisha abiria wote wanaoingia nchini kutoka sehemu mbalimbali ikiwemo Pemba au Tanzania Bara wanakaguliwa na kujua usalama wa mizigo wanayoingiza nchini.
Alisema haiwezekani kuwafanyia ukaguzi abiria katika kituo cha kwanza wanachotoka, lakini ukashindwa kufanya ukaguzi katika kituo cha pili cha kuingia abiria ikiwa ndiyo safari yake ya mwisho.
Alisema alizitaka mamlaka pamoja na vyombo vya ulinzi kuimarisha ukaguzi wa aina hiyo katika bandari zote kuu zikiwemo za Pemba na Mkokotoni, kwa upande wa Unguja.
Mkurugenzi wa Shirika la Bandari la Zanzibar, Abdallah Juma alikiri kukabiliwa na uhaba wa mashine za kisasa za kugundua vifaa mbalimbali vinavyoingizwa na abiria nchini.
Akizungumza na watendaji wa shirika la bandari pamoja na vyombo vya ulinzi katika eneo hilo, naibu waziri Masauni alitaka ulinzi uimarishwe katika vyombo vinavyotoa huduma za kubeba mizigo ikiwemo majahazi.
Alisema wahalifu wamekuwa wakibuni njia mbalimbali za kuingiza bidhaa hatari ikiwemo dawa za kulevya ambapo hutumia majahazi yanayobeba mizigo mbalimbali kuingiza dawa hizo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment