WATU WATATU WAMEKAMATWA MBEYA WAKIWA NA VIPANDE 9 VYA MENO YA TEMBO NA MIKIA 2 YA TWIGA.



Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limewakamata watu watatu wakazi wa Matwiga wakiwa na nyara za serikali ambazo ni vipande 9 vya meno ya tembo na mikia 2 ya twiga.





Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi DHAHIRI A. KIDAVASHARI amethibitisha kutokea kwa tukio ambapo amesema kuwa 09.03.2017 Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Maafisa wa TANAPA wamefanya msako wa pamoja katika Kijiji na Kata ya Lupatingatinga,Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya na kufanikiwa kuwakamata watu watatu wakiwa na nyara za serikali.

Watuhumiwa hao ni HUSSEIN KHAMIS [33] ,ISSA MLAWI [31] na ZACHARIA MUSA [36].

Watuhumiwa ni majangili.

Upelelezi unaendelea na mara baada ya kukamilika watafikishwa mahakamani.

Katika tukio la pili Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Maafisa wa Mamlaka ya Chakula na Dawa [TFDA] limefanikiwa kuwakamata wafanyabiashara wawili ambao ni ERASMO DANDA [50] Mfanyabiashara na Mkazi wa Ihanga Wilaya ya Mbarali ambaye amekamatwa akiwa na pombe kali zilizopigwa marufuku na serikali aina ya “viroba original” boksi 99 zenye thamani ya Tshs 9,768,000/= zikiwa zimehifadhiwa katika stoo yake. 

Mtuhumiwa mwingine ni JOYCE BATHLOMEO [36] Mfanyabiashara na Mkazi wa Kibaoni Wilayani Chunya,
NESTORY FILBERT [23] mkazi wa Lupatingatinga Wilaya ya Chunya, FILBERT KALUMANZILA [60] ,JOSHUA MWAKAJA [42] mkazi wa Makongolosi JACKSON ELIAS [55] mkazi wa Makongolosi Wilaya ya Chunya.

Na katika tukio la tatu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanya msako kwa kushirikiana na maafisa wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tawi la Mbeya [TFDA] katika eneo la Rujewa Kata na Tarafa ya Rujewa, Wilaya ya Mbarali na kufanikiwa kumkamata mfanyabiashara aliyefahamika kwa jina la ASUNGUKYENI MBILINYI [45] Mkazi wa Rujewa akiwa na vipodozi vilivyopigwa marufuku na Serikali.

Vipodozi vilivyokamatwa katika msako huo ni betasol lotion tube chupa 240, betasol cream chupa 144, Epiederm cream tube 12, diproson cream tube 12, carlolight cream chupa 8, cocopup chupa 20 na citrolight chupa 6. 

Jumla ya thamani ya bidhaa yote iliyokamatwa ni Tshs. 1,380,000/=.

Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi DHAHIRI A. KIDAVASHARI anatoa wito kwa wananchi kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kuwafichua wahalifu na mtandao wa wahalifu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya ili wakamatwe na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment