MKUU WA MKOA WA MWANZA AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE KUNUNUA TANI 20 ZA MTAMA.



MKUU wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela ameziagiza halmashauri zote za mkoa huo kuwa katika kipindi cha mwezi mmoja ziwe zimenunua sio chini ya tani 20 za mbegu za mtama kwa ajili ya kuzigawa kwa wakulima.



Alisema hayo wakati alipokuwa akifungua kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano katika ofisi yake.
Alisema halmashauri itakayoshindwa kutekeleza agizo hilo itachukuliwa hatua, akisisitiza kuwa serikali haiwezi kuona wananchi wake wanahangaika na kushindwa kupata mbegu hizo kwa wakati muafaka.
Alisema mwezi ujao mkoa kupitia timu yake utapita kila halmashauri kukagua mashamba ya mtama ili kujiridhisha kama agizo lake limetekelezwa kwa wakati.
Katika hatua nyingine, Mongela alisema mkoa uko kwenye mazungumzo na kampuni za bia nchini Tanzania Breweries na Serengeti Breweries kuona ni namna gani wanavyoweza kuwa na mkakati wa pamoja wa kuzalisha zao la mtama.
Alisema hali hiyo inatokana na asilimia 70 ya bidhaa zinazotumika kutengeneza bia zinatokana na zao la mtama, ambapo asilimia 95 ya zao hilo hununuliwa kutoka nje ya mkoa wa Mwanza wakati mkoa una uwezo wa kuzalisha zao hilo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment